Mtu asomapo aya zifuatazo za maandiko mara huona tatizo la dhambi linadhihirika katika maisha yake (Isaya 59:1-2; 64:6: Warumi 3:10, 23). Tunapozungumzia dhambi, kimsingi tunakuwa tunazungumzia ile ambayo humaanisha “kukosea” 1 Yohana 3:4; 5:17). Imesemwa kwamba “ingawaje wanadamu wanatofoutiana kwa kiasi kikubwa katika asili na ukubwa wa hali ya utenda dhambi, katika ukweli kwamba wote wametenda dhambi, hakuna tofauti kabisa baina ya watu bora na duni”. Pia imesemwa kwamba “Neema ya Mungu haimfai yeyote anayeshindwa kuona uhalisia na ukubwa wa udhalimu wa dhambi za mwanadamu.
Kwa kweli, peke yetu, tunasimama katika hali ya kuhukumiwa mbele za Mungu. Wakati fulani tunaimba, “Nasimama huku nashangaa mbele za Yesu Mnazareti, na nastaajabu jinsi gani angeweza kunipenda, mwenye dhambi niliye hukumiwa kuwa najisi” Bila Kristo tunastahili kutengwa na Mungu milele yote linapokuja suala rahisi la haki.
Kwa urahisi fanya hivi, endapo tunataka kuielewa neema ya Mungu, lazima tuielewe adhabu ambayo ingekuwapo bila neema. Katika makala hii, tunataka kujijuza juu ya neema ya Mungu.
NEEMA YA MUNGU INAVYOFAFANULIWA
Msingi wa neno “charis”, ambalo ndilo lililotafsiriwa neema, lina vipengele vingi ambavyo hutusaidia kukubali kazi ya neema. Katika maandishi ya Kiyunani cha kale, neno hili humaanisha kile “kilichotolewa kwa hiari, kwa kupenda au kufuatana na upendeleo”. Lilitumika pia katika mazingira ya matamshi yenye kujenga na kuinua. Kwa mfano, zingatia maneno ya Paulo katika Waefeso 4:29. Mahali penginepo neno hili kwa kiyunani lililotafsiriwa neema humaanisha, “Urafiki uliovunjika unaopelekea tendo la ukarimu,huruma, ukarimu wa upendano, kutakiana heri kiujumla” (Luka 2:52. Pia linamaanisha hali ya shukrani anayokuwa nayo mtu angeihisi kutokana na matendo ya upendeleo ambayo angeyapata. Pia tunatakiwa tuzingatie kuwa fafanuzi zote zinajikita kwamba neema ni kitu chema ajabu, kwa mpokeaji peke yake.
Katika mazingira ya kiroho kuhusiana na neema ya Mungu, neema humaanisha “isiyotokana na matendo, upendeleo wa Mungu ambao hustahili. “Katika Warumi 6:23 maneno “karama” yametokana na neno la Kiyunani “charisma” ambalo kwalo twapata “charismatic” neno ambalo kimsingi humaanisha “karama ya neema” au “karama isiyotokana na matendo”. Pia katika Tito 3:5 twaweza kuona maneno ya Paulo. Ni muhimu kutambua kuwa neema tele na huruma tulizoshushiwa ni kwa sababu “Mungu ni pendo” (1 Yohana 4:8).
UAMUZI WA MUNGU
Ni vigumu kuelewa kina cha upendo, neema na huruma za Mungu (Waefeso 3:17-19). Katika kilindi cha kina cha pendo lake, ulifanyika uamuzi wa kumtuma Kristo kabla ya “misingi ya ulimwengu” (Waefeso 1:4). Kwa uzuri wa pendo lake aliamua kumtuma “mwanawe wa pekee” Yohana 3:16). Vile vile tunatambua upendo wa Uungu, kama ulivyoonekana katika uamuzi wa Kristo kufanya kila lililowezekana ili kuwakomboa wanadamu (Yohana 1:1,2; 17:5; Wafilipi 2:6,7). “Alijidhalilisha” kama kiyunani kinavyoonyesha, “alijifanya mtupu”. Hii hutoa umbali kiasi gani Yesu alienda ili kutupa nafasi ya kuokolewa kwa neema yake.
NEEMA YA MUNGU IMEDHIHIRISHWA
Mwana wa Mungu alipokuja katika ulimwengu huu alitolewa msalabani kama “mbadala” wa dhambi zetu (1 Yohana 2:1, 2). Hili linaweza lisilete maana sana kwetu hadi tutakapoelewa kuwa “mbadala” humaanisha “upatanisho” au “kufa kwa ajili ya kupatanisha” hali inayomaanisha kukarabati, kufidia.” Neno hili linamaanisha kuigeuza ghadhabu.
Haki ya Mungu hudai uwepo wa malipo ya dhambi; ambayo Yesu alitulipia. Mwanzoni wa makala hii tuliona kwamba dhambi zetu hututenga na Mungu (Isaya 59:1-2); matokeo yake tumetengana na Mungu, tuko katika faraka. Kwa sababu ya hili, kinachohitajika ni usuluhishi. Usuluhishi ni “kuufanya upya uhusiano wa karibu”. Katika kujifunza Agano Jipya twaona ya kuwa Yesu alijitolea kuwa sadaka sadaka mbadala (2 Wakorintho 5:21). Katika aya hiyo hiyo ya 2 Wakorintho 5, Paulo alionyesha kuwa walikuwa wamepewa “huduma ya upatanisho,” iliyotoa ufahamu wa kuwezesha kupokea matendo ya neema ya Mungu (2Wakorintho 5:18).
Katika dhabihu yake ya ajabu, Kristo anatuwezesha kupata ukombozi. Katika kitabu chake cha Greek-English Lexicon, Thayer anafafanua neno ukombozi kama “kuachiliwa kunakotokana na malipo ya fidia”. “Bila Yesu sisi ni “watumwa wa dhambi” (Warumi 6:17), na kwa hivyo “tumeuzwa chini ya dhambi” (Warumi 7:14). Kama vile Paulo alivyoeleza katika maandiko yake kwa Tito, Yesu “alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote” (Tito 2:14).
Katika neema ya Mungu, kitu pekee kinachoweza kufikia gharama za ukombozi na kiwezacho kuleta upatanisho ni damu ya Kristo. Petro aliandika kuwa mwanadamu amekombolewa “….kwa damu ya thamani, kama ya mwanakondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo” (1 Petro 1:18, 19). Kuna vitu amabvyo vinaweza kukombolewa kwa fedha na dhahabu, lakini ni damu ya Kristo pekee iwezayo kumkomboa mwanadamu kutoka kwenye dhambi. Paulo alilidhihirisha hili kwa waefeso alipowambia kuwa kipindi fulani walikuwa “wafu” bila Kristo kwa sababu ya makosa na dhambi. (Waefeso 2:1,12-13)
NEEMA YA MUNGU IMEENEA NA INAPATIKANA
Hili linaonekana katika maneno ya Mtume Paulo katika Tito 2:11. Hata ingawa Kristo alijitoa kuwa dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi za wanadamu wote, haimanishi kwamba kila mtu ataokolewa. Katika Kiyunani, wazo la kuleta wokovu limejikita katika uwezekano na siyo uhalisia. Imesemwa kwamba “kama dawa iko kwenye sanduku, ndani ya chupa yenye kifuniko, mgonjwa hawezi kupona. Hilo siyo tatizo la dawa; ni tiba, lakini hakuna tiba inayoweza kufanya kazi wakati haijatumika. Hivyo, kuenea kwa karama, uwezo wa karama mahali pote, siyo ufinyu wa kiwango cha waliofikiwa kwa sababu eti kule wasikoichukua, basi manufaa yake hayatambulikani.
Ni kweli Mungu anataka watu wote waokolewe (2 Petro 3:9); walakini, katika hekima ya Mungu isiyo ukomo, Uumbaji wa Mungu ulikuwa kwamba mwanadamu awe na utashi. Twaweza kulifafanua hivi; Chukulia Mungu kwa mikono iliyoonyooshwa ameshika zawadi ya thamani kubwa; zawadi ambayo hustahili lakini unapewa bure.. Hata ingawa inatolewa bure, kwa namna yoyote hustahili kuipata. Imekufikia, lakini kuna masharti yaliyowekwa ili uipate. Unatakiwa uamue kama unaitaka ile zawadi ama la. Mungu anaweka wazi kwamba neema yake inapatikana kwa wale walio tayari kutii mapenzi yake (Mathayo 7:21; Waebrania 5:8, 9). Ingawaje ni zawadi ambayo hatuitolei jasho, hatuwezi kuokolewa mpaka tukidhi mashariti ya Mungu. Kwa hali hiyo, Mungu ametuletea neema yake sasa. Uamuzi ni wetu (Mathayo 6:24)